Majukumu Ya Kituo
Kituo cha Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika kitakuwa na majukumu yafuatayo:
i. Kuratibu ushirikiano baina ya Kituo cha Urithi wa Ukombozi wa Afrika na Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika, taasisi za kikanda na kimataifa pamoja na wadau mbalimbali wa urithi;
ii. Kuratibu uanzishwaji wa Makao Makuu ya Kituo Kikuu cha Uhifadhi wa Urithi wa Ukombozi wa Afrika nchini Tanzania;
iii. Kuanzisha na kusimamia mifumo ya kitaalamu ya ukusanyaji, uwekaji kumbukumbu, uhifadhi wa kidijitali na usimamizi wa taarifa za Urithi wa Ukombozi wa Afrika;
iv. Kuratibu uandaaji na uchapishaji wa vitabu vya historia ya ukombozi wa Afrika;
v. Kuandaa na kusimamia uandaaji wa miongozo na taratibu za utambuzi na usimamizi wa maeneo, vitu, vielelezo na nyaraka za Urithi wa Ukombozi wa Afrika;
vi. Kuratibu utambuzi, uwekaji wa kumbukumbu na utafiti wa maeneo muhimu ya kihistoria ya ukombozi wa Afrika pamoja na kuyahifadhi na kuyaendeleza;
vii. Kuanzisha na kuendesha mifumo ya programu za elimu, maonesho, maktaba, nyaraka na majukwaa ya kidijitali kwa ajili ya kuelimisha umma kuhusu historia ya ukombozi wa Afrika;
viii. Kuratibu na kuendesha makongamano, warsha, semina, maonesho, mijadala na shughuli nyingine za kitaaluma kuhusu Urithi wa Ukombozi wa Afrika;
ix. Kukuza ushirikiano na kujenga mitandao ya kitaifa, kikanda na kimataifa kati ya taasisi za urithi, vyuo vikuu, vituo vya utafiti na mashirika mengine yanayohusika na historia ya ukombozi wa Afrika;
x. Kuratibu programu za kuenzi mashujaa na mashujaa wanawake wa harakati za ukombozi wa Afrika pamoja na kuhifadhi simulizi, kumbukumbu na ushuhuda wao kwa ajili ya vizazi vijavyo;
xi. Kuhamasisha matumizi ya Urithi wa Ukombozi wa Afrika katika elimu, utafiti, utalii wa urithi, ubunifu na maendeleo ya kiuchumi na kijamii;
xii. Kuhamasisha na kuwezesha ushiriki wa sekta binafsi, taasisi za umma, washirika wa maendeleo, asasi za kiraia na wadau wengine katika uwekezaji, uhifadhi na uendelezaji wa Urithi wa Ukombozi wa Afrika;
xiii. Kuwezesha uanzishwaji na uimarishaji wa Matawi ya Kituo cha Urithi wa Ukombozi wa Afrika katika Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika pamoja na kuratibu ushirikiano baina ya matawi hayo;
xiv. Kujenga na kuendeleza uwezo wa kitaalamu wa watumishi wa Kituo, wataalamu wa urithi na wadau wengine kupitia mafunzo, kubadilishana uzoefu, utafiti shirikishi na programu za maendeleo ya kitaaluma.